Testimonies
   :: E. Tuwagiramana
   :: R. Chauganga
   :: Leah Jacob
   :: Mama Domitila
   :: Apostle Bwalya
   :: Victoria Nehale
   :: Nyisaki Chaula
 
     Resources
   :: Crossword Puzzle
   :: Music Video
   :: Audio Messages
   :: Discussions
   :: Gospel Tracts
   :: About Islam
   >Gospel Tracts
 
 
 
     Musicians
   :: Abigail Mutinda
   :: Celebrate Africa
   :: Ency Mwalukasa
   :: Charles Guzo
   :: Kirya
   :: Letwin Berebende
   :: Mamajusi Kwaya
   :: Lydia Njeri
   :: Trinity Singers
 
     Resources
   >Gospel Tracts

Your IP:
38.107.191.99
 
   :: Write to us
 
 



Charles Guzo
This testimony in English

Charles GuzoBwana asifiwe! Ninampa sifa na utukufu Bwana wetu Yesu Kristo, aishie milele na milele ambaye ameniwezesha kupata haki ya kuishi milele na milele. Yeye ni mwokozi wangu na amenisamehe dhambi zangu zote za kutokea udogo hadi sasa, na amelifuta jina langu katika kitabu cha hukumu na kuliandika kwenye kitabu cha uzima wa milele. Sasa ameniweka huru, tena huru kwelikweli.

Nikiwa katika Watangatanga Band baada ya kutoka Sparrows Band, nilikuwa nikipiga miziki ya jazz kule The New Hotel Tanga Tanzania. Nilikuwa nikishiriki kupiga drums pamoja na Paul Box raia wa Marekani. Rafiki yangu Paul yuko Marekani siku hizi na ni profesa katika Chuo Kikuu cha Utah. Nimewasiliana naye kupitia mtandao huu wa amefufuka.com nilivyo sign guest book. Alinipata akaniuliza kama ni mimi mwenyewe?

Wakati mwingine nilikuwa nikipiga gitaa na kuimba nyimbo za Kiingereza na Kiswahili, na mara nyingine nilicheza bass guiter. Band hii ilikuwa kubwa na maarufu Tanzania kwa sababu ilikuwa na wanamuziki wazungu wengi kuliko waswahili, na vyombo vilikuwa vya hali ya juu sana kwa ubora na gharama.

Hata nilipoenda Bugando Mwanza hapa hapa Tanzania kusomea Medical Laboratory Technology, niliweza kupiga muziki part-time kwenye hotel ya kitalii iitwayo New Mwanza Hotel. Nilikuwa naimba nyimbo za jazz huku nikipiga galatoni (acostic guitar).

Niliimba kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili na lugha zinginezo kwa njia ya kunakili kwa mfano; Kihispania, Kifaransa, Kiarabu, Kihindi,Guzo na Kilatini. Baada ya kurudi masomoni, niliimarisha vyombo vyangu vya muziki maana baadhi ya vyombo nilipewa kutoka Watangatanga Band. Kiongozi wa band hii alikuwa anaitwa Erling Petersern. Huyu ninamkumbuka kwani alikuwa mwalimu wangu wa guiter chords na Paul Box alinifundisha ku-roll drums. Hata hivyo, marehemu Henry Mdimu, kiongozi wa Sparrows Band na mpuliza sax alinifundisha nyimbo za zamani lakini mbinu za uimbaji nilipata kwa Watangatanga Band.

Jinsi nilivyookoka!

Nilikodishwa vyombo vyangu vya muziki kwenye mkutano wa injili. Fundi mitambo alikuwa mimi mwenyewe kwa hivyo injili ambayo nilikuwa naikimbia kila mara ilibidi niisikie. Mhubiri alitoka Kenya na jina lake ni Paulo Mbugwa. Huwa anahubiri vipindi vya redioni huko Kenya. Mwenyeji wake alikuwa Mchungaji George Barnali E.A.G.T. Makorora Tanga.

Siku ya kwanza, injili iliingia moyoni mwangu na machozi ya furaha na matumaini ya uzima wa milele yakajaa moyoni mwangu lakini nilijizuia.

Siku ya pili, nilishindwa kujizuia. Ilikuwa Mwezi wa Tisa 1994. Mhubiri Paulo Mbugwa alipouliza nani anahitaji kumpa Yesu maisha yake, nilinyoosha mikono yangu yote miwili na kutoka mbele. Kwa kweli, wahubiri walidhani labda sikuwa nimeelewa. Hivyo basi, walirudia tena mara ya pili ili kuhakikisha. Harusi

Ilipoonekana nilikuwa nimeamua kuokoka, ilikuwa ni sifa kwa Yesu mwana muziki kuokoka. Sasa nina mke na watoto watano.

Baada ya kuokoka badiliko langu lilimvuta mke wangu Elizabeth Kitiku naye akaokoka katika wiki moja. Yeye ni Afisa muuguzi katika Hospitali ya Mkoa ya Bombo. Tulianza kujuana tulipokuwa masomoni Bugando Medical Centre.

Tulikuwa ndani ya nyumba hatuna fedha wakatokea wanamuziki wa duniani wakitaka kukodi vyombo vya muziki kwa siku moja kwa kiasi cha shilingi 40,000/= nilikataa kwa vile ndani nilihukumiwa. Lakini baadaye ile gari ambayo tungesafiri nayo ikapata ajali mbaya sana kuna waliokufa na kuvunjika.

Jambo lingine: nilitumiwa galatoni mpya bila kutarajia, mke wangu akashangaa. Naomba Mwenyezi Mungu ambariki sana Dan Wolf Meyrowitsch.

Jambo lingine niliuziwa darubini nzuri (microscope) kwenye idara yangu kwa bei ya writenoff (boarded items) kwa shilingi 1,000/= tu. Huu ulikuwa muujiza mkubwa! Majirani wakawa wanahitaji huduma ikabidi nikatafute na reagent za kupimia. Siku ya kwanza tu ile 1,000/= ikarudi mara kumi! Huu ulikuwa muujiza wa Bwana.

Ikawa sinywi tena pombe akazidisha upendo wake juu yangu akagundua maisha ya wokovu yana raha akaniambia niende naye kwa mchungaji Geoge Barnali ndipo mambo yakawa mazuri zaidi. Watoto wetu walivalishwa ma-hirizi yakachomwa moto tukawa huru hakuna kuogopa wachawi tena.

Naishi hapa hapa Tanga na ninashiriki katika kanisa la Calvary Assemblies of God. Wachungaji wangu ni Apostle Dustan Maboya na Kundael Mmari.

-- Charles Guzo
To contact Charles, please write to us for his contact.
There is too much email abuse by spammers to give it here.


Charles Guzo ni mtumishi wa Mungu na mwimbaji wa nyimbo za kumsifu Mungu. Baadhi ya nyimbo alizotunga ni (Charles Guzo is a servant of God and a gospel singer. Some of the songs he has written are):

  1. Baba Yetu
  2. Haleluya
  3. Utaokoka

 

Reflections